Sehemu ya tabia:

Jawabu: Amesema Mtume Sala na amani ziwe juu yake: "Muumini aliyekamilika kiimani ni yule mwenye tabia njema zaidi kuliko wengine". Kaipokea Tirmidhiy na Ahmad.

Jawabu: 1- Kwa sababu ni sababu ya kumpenda ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

2- Ni sababu ya kupendwa na viumbe.

3- Ni kitu kizito zaidi katika mizani.

4- Na malipo huzidishwa kwa sababu ya tabia njema.

5- Ni alama ya ukamilifu wa imani.

Jawabu: Kutoka katika Qur'ani tukufu, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Hakika hii Qur'ani inaongoa kwenye yale yaliyo nyooka kabisa}. [Suratul Israai: 9]. Na kutoka katika mafundisho ya Mtume: amesema Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake: "Hakika bila shaka nimetumwa ili nitimilize tabia njema". Imepokelewa na Ahmad.

Jawabu: Wema: Ni kumchunga Mwenyezi Mungu wakati wote, na kufanya mambo mazuri na kuwafanyia wema viumbe.

Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- "Hakika Mwenyezi Mungu ameandika wema juu ya kila kitu". Imepokelewa na Imamu Muslim

Miongoni mwa namna za wema:

Ni kufanya wema zaidi katika ibada za Mwenyezi Mungu Mtukufu, Na hilo linakuwa kwa kutakasa nia katika ibada zake.

-Kuwafanyia wema wazazi wawili, kwa kauli na vitendo.

-Kuwafanyia wema ndugu wa kuzaliwa tumbo moja na wale wa karibu katika ukoo.

-Kumfanyia wema jirani.

-Kuwafanyia wema mayatima na masikini.

-Kumfanyia wema aliyekukosea.

-Kufanya wema katika mazungumzo.

-Kufanya wema katika mijadala.

-Kumfanyia wema mnyama.

Jawabu: kinyume cha wema ni kukosea (kukwaza).

Miongoni mwa makosa: Ni kuacha kutakasa nia katika ibada za Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Na kuwaasi wazazi wawili.

Kukata undugu.

Kuishi vibaya na majirani.

Kuacha kuwafanyia wema mayatima na masikini, na mengineyo katika aina za mazungumzo na matendo mabaya.

Jawabu:

1- Amana katika kuhifadhi haki za Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Aina zake: Amana katika utekelezaji wa ibada kama swala, zaka, swaumu, Hijja, na zinginezo katika zile alizozifaradhisha Mwenyezi Mungu juu yetu.

2- Amana katika kuhifadhi haki za viumbe:

Ikiwemo kuhifadhi heshima za watu.

Na mali zao.

Na damu zao.

Na siri zao, na yote ambayo watu wamekuamini.

Amesema Mwenyezi Mungu katika kutaja sifa za waliofaulu: "Na wale ambao wanavitunza vitu vyote walivyoaminiwa navyo, na wanatekeleza ahadi zao zote." [Suratul Mu'minun: 8]

Jawabu: Ni hiyana, nayo maana yake ni kupoteza haki za Mwenyezi Mungu Mtukufu na haki za watu.

Amesema Mtume Sala na amani ziwe juu yake: "Alama za mnafiki ni tatu" Na akataja miongoni mwa hizo alaama "Na akiaminiwa anafanya hiyana" Wamekubaliana Bukhari na Muslim.

Jawabu: Ni kueleza kwa namna inayoendana na uhalisia wa tukio au kukieleza kitu kama kilivyo.

Na katika namna zake:

Ukweli wakati wa mazungumzo na watu.

Ukweli katika ahadi.

Ukweli katika kila kauli na kitendo.

Amesema Mtume Sala na salamu ziwe juu yake: "Hakika ukweli unamuongoza mtu katika wema, na hakika wema unamuongoza mtu katika pepo, na hakika mtu husema kweli mpaka anakuwa mkweli" Wamekubaliana Bukhari na Muslim.

Jawabu: Ni uongo, nao ni kinyume cha uhakika, na miongoni mwake, ni kuwaongopea watu, kutotimiza ahadi, na kutoa ushahidi wa uongo.

Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- "Na Tahadharini sana na uongo! kwani uongo unapelekea katika uovu, na hakika uovu unampelekea mtu kuingia Motoni, na hatoacha mtu kuendelea kusema uongo, na kuutafuta uongo mpaka ataandikwa mbele ya Mwenyezi Mungu kuwa ni muongo". Wamekubaliana Bukhari na Muslim. Amesema Mtume Sala na salamu ziwe juu yake: "Alama za mnafiki ni tatu" Na akataja miongoni mwake "Akizungumza husema uongo, na akitoa ahadi hatimizi". Wamekubaliana Bukhari na Muslim.

Jawabu: Kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu Mtukufu.

- Kusubiri kutoyaendea maasi.

-kusubiri juu ya makadirio ya Mwenyezi Mungu yaumizayo, na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kila hali.